Siri ya Jina la Mwezi wa Muharram, Maana za Miezi 12 ya Kiislamu na Wajibu wa Muumini

Sifa zote njema zinamstahiki Allah (Subhanahu wa Ta'ala), Mola wa walimwengu wote, aliyekadiria nyakati na akajaalia miezi kuwa kipimo cha ibada na maisha ya mwanadamu. Swala na salamu zimfikie mwalimu wa ummah, Mtume Muhammad (Swallah Llahu 'alayhi wa sallam), kizazi chake na maswahaba zake waliotunza misingi ya dini hii kwa uaminifu mkubwa. Kila mfumo thabiti wa maisha kuna alama zake za utambulisho, na katika Uislamu, Kalenda ya Hijriyah ndio dira yetu kuu ya nyakati. Hata hivyo, Waislamu wengi wamezoea kutumia majina ya miezi hii bila kufahamu chimbuko lake, maana zake, na wajibu uliopo ndani ya kila mwezi. Kupitia makala hii kabambe kutoka jukwaa lenu la AMAN VISSION , tutazama kwa undani kuelewa siri iliyopo nyuma ya jina la mwezi wa Muharram , maana za miezi yote 12, na mambo anayotakiwa kuyatekeleza Muumini katika kila kituo cha mzunguko wa mwaka. Siri ya Jina Muharram: Je, Lilitokana na Tukio Gani? Neno "Muharram" (المحرّم) kihisaba...

Mbona Shule za Kawaida Tunalipa Lakini Madrasa Tunasita? Nini Kifanyike Kuamsha Wazazi?


AMAN VISSION

Mjadala wa Wazi: Mchango wa Wazazi katika Kufanikisha Masomo ya Madrasa
Uzoefu unaonesha kuwa wazazi wengi wamekuwa weepesi sana kugharamia na kufuatilia maendeleo ya watoto wao kwenye shule za kawaida (Academic Schools), lakini wanakuwa wazito sana linapokuja suala la kuchangia huduma na kufuatilia masomo ya watoto wao wanapokuwa Madrasa.

Jukwaa la AMAN VISSION chini ya uongozi wa Mwalimu wa Kiislamu: Aman Ismail Hussein, linakaribisha maoni yako leo: Je, nini kifanyike ili kuamsha ari ya wazazi kuwa mstari wa mbele kufuatilia na kugharamia elimu ya dini ya watoto wao kwa uzito ule ule wa shule za kawaida?
TAARIFA BINAFSI
MCHANGO WAKO WA MAONI

Comments