Siri ya Jina la Mwezi wa Muharram, Maana za Miezi 12 ya Kiislamu na Wajibu wa Muumini

Sifa zote njema zinamstahiki Allah (Subhanahu wa Ta'ala), Mola wa walimwengu wote, aliyekadiria nyakati na akajaalia miezi kuwa kipimo cha ibada na maisha ya mwanadamu. Swala na salamu zimfikie mwalimu wa ummah, Mtume Muhammad (Swallah Llahu 'alayhi wa sallam), kizazi chake na maswahaba zake waliotunza misingi ya dini hii kwa uaminifu mkubwa. Kila mfumo thabiti wa maisha kuna alama zake za utambulisho, na katika Uislamu, Kalenda ya Hijriyah ndio dira yetu kuu ya nyakati. Hata hivyo, Waislamu wengi wamezoea kutumia majina ya miezi hii bila kufahamu chimbuko lake, maana zake, na wajibu uliopo ndani ya kila mwezi. Kupitia makala hii kabambe kutoka jukwaa lenu la AMAN VISSION , tutazama kwa undani kuelewa siri iliyopo nyuma ya jina la mwezi wa Muharram , maana za miezi yote 12, na mambo anayotakiwa kuyatekeleza Muumini katika kila kituo cha mzunguko wa mwaka. Siri ya Jina Muharram: Je, Lilitokana na Tukio Gani? Neno "Muharram" (المحرّم) kihisaba...

Maktaba ya Vitabu Na Nyaraka Rasmi


MAKTABA YA VITABU NA NYARAKA RASMI

Digital Resources, Schedules & Academic Rules
Nyaraka za Taaluma, Ratiba na Sheria za Mfumo
Mtaala wa elimu wa AMAN VISSION umesimama juu ya misingi thabiti ya kitaaluma inayoratibu Shule na Vyuo vya Kiislamu. Nyaraka hizi zinajumuisha ratiba za vipindi vya kila siku na mgawanyo wa mihula. Kupitia mwongozo wa sheria, mfumo unaweka bayana taratibu za mahudhurio, nidhamu, uendeshaji wa kambi (bweni), pamoja na majukumu ya wanafunzi wa mtandaoni (online) na wa kutwa ili kuhakikisha ufanisi wa kielimu na kiakhlaq unapatikana kwa kiwango cha juu.

Ratiba ya Masomo: TAMHIID

Ratiba na Vipindi

Mchanganuo kamili wa vipindi vya kila wiki, muda wa masomo na mtiririko wa mihula miwili kwa wanafunzi wa Ngazi ya Kwanza (Tamhiid).

📥 Pakua Ratiba (Tamhiid)

Ratiba ya Masomo: MUTAWASSITWAH

Ratiba na Vipindi

Ratiba rasmi ya darasani na mtandaoni kwa ajili ya wanafunzi wa Ngazi ya Kati (Mutawassitwah) wanaosoma mtaala wa mwaka mmoja.

📥 Pakua Ratiba (Mutawassitwah)

Ratiba ya Masomo: THAANAWIY

Ratiba na Vipindi

Mwongozo wa masomo, vipindi na mihula miwili ya ufundishaji wa kina kwa wanafunzi wa Ngazi ya Juu (Thaanawiy).

📥 Pakua Ratiba (Thaanawiy)

Sheria na Kanuni za Mfumo wa Elimu AMAN VISSION

Mwongozo wa Taaluma na Nidhamu

Nyaraka rasmi inayoeleza sheria za shule na vyuo vya Kiislamu, taratibu za ada, miongozo ya nidhamu kwa wanafunzi wa Kutwa (Day), Kambi (Bweni) na wale wa Mtandaoni (Online), pamoja na maadili ya jumla yanayopaswa kuzingatiwa wakati wote wa masomo.

📥 Pakua Mwongozo wa Sheria na Taratibu zote (.PDF)
Ngazi ya Kwanza: Tamhiid (Mwanzo)
Muda wa Masomo: Mwaka 1 (Mihula Miwili / Semesters 2)
Lengo Kuu: Hii ni ngazi ya msingi mkuu na utangulizi wa elimu ya Kiislamu. Inalenga kumjengea mwanafunzi uwezo thabiti wa kusoma Qur'ani kwa tajwiid sahihi tangu hatua ya herufi, kujua misingi ya itikadi (Aqiidah), kujifunza fikra sahihi za ibada za kila siku kama vile Twahara na Swala, na kuanza kupata msamiati wa Lugha ya Kiarabu pamoja na misingi ya uandishi (Imla).

Al-Qaaidat Nnooraaniyyah

Qur'aan na Tajwiid

Herufi na matamshi sahihi ya maneno ya Qur'an Tukufu.

📥 Pakua Kitabu

Tuhfatul Atwfaal

Qur'aan na Tajwiid

Misingi ya Tajwiid ikiwemo sheria za Nun Sakina na Tanween.

📥 Pakua Kitabu

Thalaathatul Usool

Aqiidah na Tawhiid

Misingi mitatu mikuu: Kumjua Mola wako, kumjua Mtume wako, na kuijua Dini yako.

📥 Pakua Kitabu

Al-Fiqhul Muyassar

Fiqhi na Al-Usuul

Misingi ya ibada za kila siku, ikizingatia sehemu ya Twahara na Swala.

📥 Pakua Kitabu

Khulaaswat Nnuurul Yaqiin (Juzuu 1)

Taariikh na Siirah

Historia ya maisha ya Mtume Muhammad (S.A.W) katika kipindi cha Makka.

📥 Pakua Kitabu

Duruus LLughatul Arabiyyah (Kitabu 1)

Lugha ya Kiarabu

Misingi ya kwanza ya mazungumzo na herufi za Kiarabu.

📥 Pakua Kitabu

Qawaaidul Imlaa

Lugha ya Kiarabu (Imla)

Misingi rahisi na ya mwanzoni ya uandishi na imla ya Kiarabu.

📥 Pakua Kitabu
Ngazi ya Pili: Mutawassitwah (Kati)
Muda wa Masomo: Mwaka 1 (Mihula Miwili / Semesters 2)
Lengo Kuu: Ngazi hii inamvusha mwanafunzi kutoka hatua ya awali kuelekea kiwango cha kati cha uchambuzi. Hapa mwanafunzi anasoma sheria za ndani zaidi za sarufi ya Kiarabu (Nahwu na Swarfu) ili kuanza kuelewa vitabu vya kielimu vilivyoandikwa kwa lugha asili. Pia masomo ya Fiqhi yanapanuka kupitia misingi ya kisheria (Al-Usuul), na masomo ya Tauhidi yanajikita katika kulinda na kuelewa vyema mipaka ya imani.

Hidaayatul Mustafiid

Qur'aan na Tajwiid

Sheria kamili za Tajwiid zilizopangwa kwa mfumo wa maswali na majibu.

📥 Pakua Kitabu

Al-Arba'iina Nnawawiyyah

Hadiith na Sunnah

Misingi mikuu na miongozo ya dini kupitia hadithi arobaini za Imam An-Nawawi.

📥 Pakua Kitabu

Matnul Ghaayat Wattaqriib

Fiqhi na Al-Usuul

Kitabu cha Abi Shujaa'h kinachofundisha Fiqhi ya kina ya ibada na muamalat.

📥 Pakua Kitabu

Al-Waraqat

Fiqhi na Al-Usuul

Kitabu mashuhuri cha Imam Al-Juwayni kinachotoa utangulizi wa misingi ya Fiqhi.

📥 Pakua Kitabu

Al-Qawa'id Al-Arba'

Aqiidah na Tawhiid

Kanuni nne muhimu katika kuelewa na kujiepusha na shirki (ushirikina).

📥 Pakua Kitabu

Kitab at-Tawheed

Aqiidah na Tawhiid

Ufafanuzi wa kina na thabiti kuhusu Tauhidi ya ibada pekee kwa Allah.

📥 Pakua Kitabu

Khulaaswat Nnuurul Yaqiin (Juzuu 2 & 3)

Taariikh na Siirah

Historia ya Mtume (S.A.W) kipindi cha Madina pamoja na historia ya Khilafa.

📥 Pakua Kitabu

Al-Ajruumiyyah

Lugha ya Kiarabu (Nahwu)

Kitabu kikuu cha misingi ya sarufi ya lugha ya Kiarabu (Nahwu).

📥 Pakua Kitabu

Matnul Binaa wal-Asaas

Lugha ya Kiarabu (Swarfu)

Kitabu kinachofundisha mfumo na mnyambuliko wa maneno ya Kiarabu (Swarfu).

📥 Pakua Kitabu

Kitaabul Kabaair

Adyaan na Daawah

Kitabu kinachofundisha madambi makubwa ili mwislamu aweze kujiepusha nayo.

📥 Pakua Kitabu

Adda'wah ila Llaah

Adyaan na Daawah

Mbinu, hekima na busara za mwanzo za ulinganizi na uenezaji wa heri.

📥 Pakua Kitabu
Ngazi ya Tatu: Thaanawiy (Juu)
Muda wa Masomo: Mwaka 1 (Mihula Miwili / Semesters 2)
Lengo Kuu: Hiki ni kiwango cha juu cha Maandalizi ya Kida'wah na Uongozi wa Kijamii. Wanafunzi wanajikita kwenye vitabu vikubwa vya Hadithi zenye hukumu (Ahkam), kuelewa kwa mapana masuala ya Aqiidah ya Ahlus Sunnah, kusoma historia za kina za mitume na wasifu wa Mtume (Siirah), pamoja na kupata ujuzi thabiti wa usemi, uandishi wa juu wa Kiarabu, kulinganisha dini, na mbinu za kiungozi katika jamii.

Matnul Jazariyyah

Qur'aan na Tajwiid

Kitabu cha ushairi kinachofafanua kwa kina sifa na matamshi sahihi ya herufi za Qur'an.

📥 Pakua Kitabu

Umdatul Ahkaam

Hadiith na Sunnah

Mkusanyiko wa hadithi za kisheria (Ahkam) zilizochukuliwa kutoka vyanzo sahihi kabisa.

📥 Pakua Kitabu

Buluughul Maraam

Hadiith na Sunnah

Kitabu cha hadithi kilichopangwa kwa kufuata milango ya kisheria na kifiqhi.

📥 Pakua Kitabu

Manhaj Ssaalikiin

Fiqhi na Al-Usuul

Ufafanuzi wa Fiqhi ya kielimu na kivitendo isiyofungamana na upande wa madhehebu.

📥 Pakua Kitabu

Al-Aqiidah Al-Waaswitwiyyah

Aqiidah na Tawhiid

Itikadi sahihi ya Ahlus Sunnah wal Jama'ah juu ya Majina na Sifa tukufu za Allah.

📥 Pakua Kitabu

Ar-Raheequl Makhtoom

Taariikh na Siirah

Kitabu kinachotoa wasifu na historia ya kina kabisa ya maisha ya Mtume (S.A.W).

📥 Pakua Kitabu

Qiswasul Anbiyaai

Taariikh na Siirah

Historia na kisa cha kuvutia cha Mitume waliotangulia kilichoandikwa na Ibn Kathiir.

📥 Pakua Kitabu

Al-Qiraa'at Rrashiidah

Lugha ya Kiarabu

Kukuza uwezo wa kusoma, kupata msamiati, matumizi ya usemi na uandishi wa juu.

📥 Pakua Kitabu

Al-Milal wa Nnihal

Adyaan na Daawah

Kitabu kinachofundisha kuelewa makundi, madhehebu, na kulinganisha dini nyingine.

📥 Pakua Kitabu

Comments